Posts

MAISHA NDIVYO YALIVYO

Image
Lazima kuwe na Equity and Justice . 

UMUHIMU WA BUSINESS PLAN KWA MFANYABIASHARA

Image
UMUHIMU WA BUSINESS PLAN KWA MFANYABIASHARA. Business Plan (mpango biashara) ni nini? Business Plan ni taarifa iliyoandikwa ambayo huonyesha lengo la biashara husika kwa kuonyesha hatua muhimu za kupitia ili kufikia lengo. Hapa unapata picha kuwa, ni wapi ulipo, unaenda wapi na jinsi gani utafika ulipo kusudia kufika. *Umuhimu wa business plan kwa mfanya biashara.* Tuangalie umuhimu wa mpango biashara kwa mfanya biashara. Mpango biashara ina umuhimu mkubwa sana kwa mfanya biashara /mjasiriamali yeyote ambapo faida zake ni kama ambavyo tutazitazama hapa chini. i) Humsaidia mfanya biashara kuepukana na uwezekano wa kuingia katika biashara yenye uwezekano wa kufa. Kama tulivyo ona katika makala zetu zilizo tangulia, business plan inakuwa kama ramani ya kukuonyesha njia sahihi ya kupitia. Hivyo ukiitumia kwa usahihi utakuwa na biashara au mradi endelevu. ii) Humsukuma mfanyabiashara kuongeza umakini katika usimamizi wa biashara yake. Muda, juhudi, utafiti na nidhamu hutumika ha...

UMUHIMU WA BUSINESS PLAN

Image
*UMUHIMU WA BUSINESS PLAN.* Business Plan (mpango biashara) ni nini?  Business Plan ni taarifa iliyo andikwa ambayo huonyesha lengo la biashara husika kwa kuonyesha hatua muhimu za kupitia ili kufikia lengo. Hapa unapata picha kuwa, ni wapi ulipo, unaenda wapi na jinsi gani utafika ulipo kusudia kufika. *Umuhimu wa business plan* i)  Mpango huo unaelezea njia ambayo mfanya biashara au mjasiriamali anayopaswa kupitia kipindi chote cha uendeshaji wa biashara yake. Katika biashara lazima kuwepo na kanuni na taratibu, hivyo basi ili biashara yako ikue lazima kuwe na njia unazopaswa kupitia, na kupitia business plan kila kitu kitakuwa kimejipambanua humo. ii) Husaidia wawekezaji, watu wa mabenki na wafadhili wengine kuelewa na kumkubali mfanya biashara kwa ajili ya uwekezaji wao katika biashara yake.  Lazima utambue kuwa popote utakapo hitaji kwenda kupata msaada wa kuongeza mtaji (mkopo) kwa ajili ya kukuza biashara yako lazima uwe na mpango kazi huu ili kumuwezesha hu...

SULUHISHO LA BIASHARA YAKO NA NDOTO YAKO.

Image
SULUHISHO LA BIASHARA YAKO NA NDOTO YAKO. Watu wengi tumekuwa tukishindwa kutimiza ndoto zetu kutokana na kutokuwa na mpango kazi na mikakati mizuri. Nyumbani Business Plan LTD imelitambua hilo na imeamua kukuletea huduma mpya kwa ajili yako. Sasa utapata Huduma ya kuandikiwa BUSINESS PROPOSAL kwa ajili ya kukuwezesha kupata mkopo au msaada wowote kwa ajili ya kuendeleza biashara yako. Tunao wataalamu waliobobea katika fani hii. Pia tunatoa huduma ya kuandika BUSINESS PLAN, tunakualika kuweza kupata huduma hii ambayo inatolewa kwa viwango vya hali ya juu kabisa. Huduma hizi zinatolewa kwa gharama ndogo kabisa kinyume na unavyofikiria. Wasiliana nasi kupitia namba +255 753 183 583 / +255 785 494 456 au tutumie barua pepe kupitia, nyumbanibusinessplan@gmail.com KARIBUNI SANA. Huduma bora ndio kipaumbele chetu.

THERE IS NO FUTURE IN THE PAST

Image
THERE IS NO FUTURE IN THE PAST. Ukitaka kufanikiwa usiangalie nyuma yako kunanini na ulishindwa mara ngapi. Siku zote kukaa Chini nakuanza kujuta kwa makosa uliofanya uko nyuma nikupoteza muda, huo muda Utumie kwa kupanga ya kesho. Bahati nzuri Mungu alitujalia kusahau, ivyo siku zote sahau ya nyuma na waza yale ya mbele yako. Maisha bora ya mbele hayawezi kuja kama akili yako imebeba kushindwa kwa nyuma. Binadamu yeyote anayeweza kupoteza muda wake wa leo kwa kulaumu mabaya ya jana, kesho atapoteza muda akilaumu mabaya ya leo. Tambua ya kuwa, "hakuna awezaye kurudi nyuma na kuanza upya, bali waweza kuanza leo na kutengeneza maisha yako ya kesho" Kadri unavyofikiria ya nyuma ndivyo unavyochelewa kufika mbele zaidi. Penda zaidi ndoto yako ya kesho kuliko historia yako ya jana,maana hatima yako siku zote iko mbele na sio nyuma. Siku zote utashindwa kwa kuendekeza mambo yaliopitwa na wakati maana utakuwa unatumia ujuzi uliopitwa na wakati. "Habari njema ya siku ni ...

FAIDA ZA MMEA WA GINSENG

Image
FAIDA ZA MMEA WA GINSENG. Ginseng ,au maarufu kama “king of herb” (mfalme wa mimea). Mmea huu umekuwa moja ya maajabu ya dunia kutokana na uhodari wake katika matibabu.  Mmea huu unapatikana hasa kaskazini  mwa America na Mashariki mwa Asia(hasa kaskazini mwa china,Japani na Korea) hasa maeneo yenye baridi. Kuna aina kuu mbili za mmea huu : American Ginseng(Panax quinquefolium) na Asian Ginseng au China ginseng(Panax ginseng) American Ginseng ni  zenya asili ya ubaridi( Ying energy) na Asian Ginseng ni zenye asili ya ujoto(Yang ginseng) , hivyo  basi watu wenye asili ya ubaridi  au waishio maeneo ya baridi  wanashauriwa kutumia Asian ginseng ili waweze kupata joto na wale wenye asili ya joto au waishio maeneo ya joto wanashauriwa kutumia American ginseng kwaajili ya kuongeza baridi katika mili yao. Vinginevyo matatizo makubwa yanaweza kujitokeza hasa kwa watu wenye shinikizo la damu . Mbali na utofauti wote huo lakini mimea yote ina kiungo ...

NI ZAMU YAKO MKAZI WA MWANZA 09/07/2016.

Image
Swali la kujiuliza ni je, unandoto na unatamani itimie, ila hujui jinsi ya kuitimiza? Basi ungana nami tarehe 09/07/2016 ndani ya GOLD CREST HOTEL - Mandela hall,  kuanzia saa sita mchana mpaka saa kumi na moja jioni. Nitakuwepo kukufundisha mbinu mbalimbali za kibiashara na kukutengenezea misingi ya kutimiza ndoto yako.  1. Nitakufundisha mbinu za kuweza kutoka kuitegemea ajira tu na kuanza kujiajiri.  Pia 2. Nitakuonyesha mbinu mbalimbali za kuanzisha biashara. Pia nitakuwa na wenzangu ambao watakusaidia  kukupatia maarifa mbali mbali yatakayo fungua akili yako na kuwa mpya na kisha kuanza kutimiza ndoto yako. Kwaajili ya kukuwekea nafasi, basi tuma jina lako mapema kwenda namba +255 785 494 456. Maana watu watakuwa wengi Ivyo Tuma jina mapema ili tukuwekee nafasi. Unaruhusiwa kumualika ndugu, jamaa na rafiki yako ili nao waje wapate elimu hii BURE. KARIBU SANA.

HABARI NJEMA KWAKO MWANA DAR ES SALAAM

Image
HABARI NJEMA KWAKO MWANA DAR ES SALAAM. Najua kila mtu anatamani kuniona na kujifunza mengi kutoka kwangu.  Sasa fursa ni hii.  NJOO UBUNGO PLAZA, GHOROFA YA PILI, OFFICE NAMBA 202. Nitakuwepo kukufunza juu ya uanzishaji biashara kwa mitaji midogo.  Najua kila mtu anatamani kuwa na biashara yake ila tatizo kubwa limekuwa ni mitaji. Sasa basi, njoo siku ya Ijumaa, Tarehe 24/06/2016 Kuanzia saa 12:00 Mchana mpaka saa 05:00 Jioni. Ili nikupe mbinu hizi adimu kabisa. Njoo, kiingilio ni bure na nitakufundisha bure. Unaruhusiwa pia kuja na mwenzako. By,  Frank A. Ndyanabo - FAN

TANGAZO LA AJIRA

Image
TANGAZO LA AJIRA. NYUMBANI BUSINESS PLAN ENTERPRISES Inakutangazia nafasi ya kazi katika idara ya afisa mauzo kwa watu wote waishio MWANZA. SIFA ZA MUOMBAJI. ••Awe ni muhitimu wa kidato cha nne Au sita. ••Awe na shahada,stashahada au cheti cha Masoko(marketing), Sayansi ya jamii(sociology), usimamizi wa biashara(business administration), fedha (finance), kibenki(banking) KAZI ZA AFISA MAUZO. 1.Kutafuta na kutengeneza masoko mapya ya bidhaa. 2.Kuandaa taarifa ya mauzo kila siku, kwa wiki na mwezi. 3.Kufuatilia na kukusanya mauzo ya kila siku. 4.Kutoa taarifa ya utendaji kazi kwa msimamizi(supervisor) wake kila siku. MSHAHARA MNONO UTATOLEWA TUMA MAOMBI: Tuma maombi yako kwenda kwa Afisa Utumishi wa Nyumbani Business Plan. Email: nyumbanibusinessplan@gmail.com Kwa Mawasiliano zaidi. • +255 753 183 583 • +255 684 459 947 MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 30/06/2016

ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO.

Image
ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO. SEHEMU YA 2. Karibu katika mwendelezo wa mada yetu iliyotangulia ikiwa na sehemu ya kwanza na leo tuko katika sehemu ya pili. Kila mtu anatamani maisha yake yabadilike kutoka alipo na kusonga mbele zaidi. Ila maisha hubadilika pale tu unapotaka yabadilike. Na ili yaweze kubadilika lazima ukubali kupigika kwa ajili ya kuyafanya yabadilike.  Huwezi kulala na kuamka ukakuta yamebadilika. Kwa leo hebu tujifunze njia zingine : 6. Achana na mahusiano yenye kukuumiza. Watu wengi naweza sema ni ving'ang'anizi kwa mambo yasiyo na tija.  Haimaanishi kuwa, kwakuwa umekuwa na mtu au umekuwa ukifanya jambo fulani kipindi cha nyuma basi ni lazima uwe nae au uendelee na mambo hayo maishani mwako. Kukosa jambo fulani ulilolizoea haimaanishi kuwa lazima ulipate.  Au kumkosa mwenzako aliye kuumiza hapo awali haimaanishi kuwa lazima uwe nae maishani mwako.  Kukikosa kitu cha awali ni nafasi nzuri kwako kupata muda wa kusonga mbele k...

UNAJIFUNZA NINI KUTOKA KWA BINTI GETRUDE CLEMENTI?

Image
UNAJIFUNZA NINI KUTOKA KWA BINTI GETRUDE CLEMENTI? Getrude Clement ni binti kutoka Jijini Mwanza, nchini Tanzania.  Na anasoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari Mnarani, ilioko nje kidogo ya mji takribani km 10 au zaidi kutoka mjini. Shule iyo ni ya serikali ni moja kati ya shule za kata zilizoanzishwa kipindi hicho. Getrude ana umri wa miaka 16. Alipata fursa ya kipekee kuongea kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa, akikaribishwa na Mhe. Ban Ki Moon, katibu mkuu wa umoja wa Mataifa kama muwakilishi wa watoto na vijana wote duniani kwa ajili ya kuzungumzia maswala ya mazingira na uchafuzi wake. Baba yake ni Kinyozi na mama yake ni mfanya biashara mdogo mdogo wa nyanya na vitunguu. Getruda Clement, aliweza kuushangaza ulimwengu jinsi alivyo simama mbele ya viongozi mbali mbali nakuweza kuhutubia bila wasi wasi na kwa kujiamini kupita kiasi.  Ujasiri alio nao binti huyu ndio umenifanya niandike maneno haya ili uweze kujifunza kitu fulani. Wewe kama mfuatiliaji mzuri wa...

ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO.

Image
ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO. SEHEMU YA 1: Kila mtu anatamani maisha yake yabadilike kutoka alipo na kusonga mbele zaidi.  Ila maisha hubadilika pale tu unapotaka yabadilike. Na ili yaweze kubadilika lazima ukubali kupigika kwa ajili ya kuyafanya yabadilike.  Huwezi kulala na kuamka ukakuta yamebadilika. Leo nimeamua kukuletea njia zitakazo fanya maisha yako yabadilike kikamilifu endapo utayazingatia.  Siku zote ndoto yangu mimi Frank A. Ndyanabo - FAN ni kuona kila ninacho kifanya kinaleta matunda chanya kwa watu hasa wewe unayesoma na kufuatilia makala zangu hapa kila siku.  Ila ndoto hii na furaha yangu haiwezi kukamilika kama hautawashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako ili na wao wapate ujumbe huu. Sasa hebu njoo tutembee pamoja tujifunze mambo haya. 1. Ondoa mambo mabaya maishani mwako. Ukiona kitu fulani hakikuongezei thamani au hakina manufaa maishani mwako huna budi kukiacha.  Huwezi kupata maisha mapya bila kukubali kuachana na ...

MATENDO NI TIBA YA WOGA.

Image
MATENDO NI TIBA YA WOGA. Hii ndio dawa pekee ya kutibu ugonjwa wa woga ndani yako.  Pindi tunapotaka kufanya jambo fulani utakuta tunakabiliwa na woga. Woga ni kitu kibaya sana katika maisha yetu ya kila siku. Jiulize ni mambo gani umeshindwa kuyafanya kwa sababu ya woga. Siku zote ukitaka kushinda jambo kwanza ondoa woga ndani yako.  Na ili kufanikisha jambo lako jiulize ni kitu gani ufanye ili kukabiliana na woga uliopo ndani yako. Jibu utakalolipata litumie kukabiliana na adui huyo woga.  Utakuwa umepata muarobaini wa mafanikio yako. Weka mfumo mpya sasa wa maisha yako, utakaokupa mwanga sahihi katika maisha yako.  Utakuwa umekutana na fursa nyingi katika maisha yako ila woga umekufunika na kuiteka akili yako.  Sasa ni wakati wa kukataa hali hiyo na kuamua kutenda. Nyanyuka tutembee pamoja sasa. By: Frank A. Ndyanabo - FAN

VYAKULA HIVI VITAKUSAIDIA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATIZO YATOKANYO NA KUKUA KWA TEZI DUME.

Image
VYAKULA HIVI VITAKUSAIDIA KUONGEZA UFANISI WA VICHOCHEO VYA KIUME (TESTOSTERONE) NA KUKINGA DHIDI YA MATATZO YATOKANAYO NA KUKUA KWA TEZI DUME. Kichocheo cha testosterone au kwa Kiswahili , japo huusishwa zaidi na upande wa mwananume ni muhimu kwa afya ya pande zote mbili yaani mwanamke na mwanamme, pia kadiri umri unavoenda mbele basi kiwango cha uzalishaji wa kichocheo cha testerone upungua, kupungua kwa kichocheo hiki kunaambatana na ukuaji wa tezi dume (prostate gland),kupotea kwa nywele na pia saratani mfano saratani ya tezi dume. KAZI KUBWA YA KICHOCHEO HIKI NI KUONGEZA MSUKUMO NA HAMU YA TENDO LA NDOA, KUIMARISHA MISULI NA MIFUPA MWILINI. NINI KINAHITAJIKA ILI KUZALISHA KICHOCHEO CHA TESTOSTERONE? Ili kuhakikisha uzalishaji wa kichocheo cha kiume unafanyika mwili unahitaji virutubisho au viini lishe mbalimbali, baadhi ya viini lishe hivyo ni madini ya ZINC na vitamin D3,  vitamini D inaweza kuzalishwa na mwili pale ngozi yako inapokutana na mwanga wa jua, hapa nazungumzi...

UMRI WAKO SIO KIKWAZO.

Image
Watu wengi tumekuwa tukipata kigugumizi juu ya maamuzi yetu katika kuzielekea ndoto zetu.  Wapo tunaofikiria umri wetu kutujengea vikwazo mbele yetu.  Umri wako kuwa mkubwa sio sababu ya kukuzuia kutimiza ndoto yako.  Nimekuwa nikikutana na watu mbali mbali na kuwashirikisha juu ya fursa za kuwaletea maendeleo lakini hutanguliza swala la umri mbele.  Utasikia mtu anakwambia, "mimi umri umekwenda nimeisha jichokea na karibia nitakufa"  Aliyekwambia utakufa kesho au baada ya mwaka mmoja ni nani?  Umri wa uzalishaji kwa mwanadamu hasa Tanzania ni miaka 60.  Sasa utakuta mtu ana miaka 40 anakwambia umri wake umeenda na hawezi kufanya jambo lolote kwa sababu ya umri.  Sasa kama una miaka 40, hujui kuwa bado una miaka 20 mbele?  Kwa maana hiyo umeisha tumia 50% ya maisha yako katika utafutaji hapa duniani. Toka ulivyo timiza miaka 20 nakuanza kujitengenezea maisha, ulikuwa na jukumu la miaka 40 mbele, hivyo bado unadaiwa asilimia 50 mbele yako....

JIFUNZE JAMBO HILI KILA SIKU.

Image
Mzee mmoja alianza hofia kuwa yawezekana mkewe kaanza matatizo ya kutosikia vizuri.Hivyo ikambidi amtafute daktari wa familia na kumsimulia mkasa mzima. Baada ya daktari kumsikiliza yule mme vizuri, akamwambia kuwa sasa atahitaji akirudi nyumbani amfanyie jaribio moja mkewe ili majibu yake yaweze kumpa dokta mwanga wa kumsaidia kulitambua tatatizo na yule mama apone. Daktari akamwambia, “ ukirudi nyumbani simama futi 40 kutoka kwa mkeo na kwa sauti ya mazungumzo ya kawaida ongea neno ili uone kama atasikia na kama hatasikia simama karibu futi 30 ukimsogela , kama hatishoshi ongeza zaidi futi 20 mpaka atakapo kusikia” Jioni yake mzee akiwa sebuleni na mama akiwa jikoni anaandaa chakula cha jioni, baba akiwa sebuleni akamwita mkewe na kuuliza, “Mpenzi tuna kula nini leo jioni?” lakini mke hakujibu. Mzee akazidi kusogea futi 30 karibu akamuuliza tena, “Mpenzi tuna kula nini leo jioni?” lakini pia mke hakujibu, mzee akasogea tena fu...

ZINGATIA HAYA KILA SIKU.

Image
ZINGATIA HAYA KILA SIKU. Yaweza kuwa unayafahamu ila hujui umuhimu wake, au unajua ila unayachukulia kawaida sana.  Lazima ufikie mahali ujiulize ni kwa kiasi gani unazitumia mbinu hizi kimaendeleo. Hizi ndio waswahili usema "nondo nzito"  ila mimi nasema ni "funguo tatu muhimu katika maisha yako"  funguo hizi ukipoteza moja wapo basi usitegemee muujiza, Maana mafanikio hayamfuati mtu kama muujiza bali mtu mwenye ndio uyafanya yamtokee kama muujiza kwake.  Na funguo hizi ndio za kutumia ili ufikie pale ulipopalenga. MTANGULIZE MUNGU KILA SIKU: Najua kila mtu ananjia yake ya kuabudu, uwe Mwislam au mkristu unamuabudu Mungu alie juu, basi tambua kuwa ata uwe mjanja namna gani Mungu ndio kilakitu.  Huwezi kufanikiwa bila kumuweka mbele.  Nakumbuka wakati nikiwa shuleni, na nikiwa kiongozi wa dini kwa wanafunzi kimkoa tulikuwa na usemi wetu kuwa "God.... first, education..... Second"  hii inamaana kuwa katika mambo yote utakayoyafanya lazima Mungu umtan...

HACHA KUIHUKUMU NAFSI YAKO

Image
HACHA KUIHUKUMU NAFSI YAKO. Kila mtu analo jambo la kufanya na tunayo malengo ya kutimiza, ila tatizo ni kuwa mioyo yetu imejaa hukumu zisizo za msingi ndio maana tunashindwa kutimiza malengo yetu.  Tunatanguliza kushindwa, aliekwambia kuwa huwezi kumiliki biashara yako nani, nani alikwambia kuwa huwezi kumiliki kampuni?  Nani alikwambia huwezi kuwa kiongozi bora, unafikiri mafanikio watu wanazaliwa nayo?  Yote yanatafutwa hapa hapa duniani.  Hacha kujihukumu bure kuwa huwezi jambo fulani,kwani wewe ni nani usiweze, wanaoweza wana nini cha ajabu? Biashara zetu zinashindwa kustawi kutokana na minyororo iliopo ndani yetu maana tumeifunga kisawa sawa.  Mtu wazo la kufanya biashara au jambo fulani unalo ila hutaki kufanya unategemea nani akufanyie sasa, au unataka jirani yako aje afanye badala yako?  Hachana  na mawazo hayo ya kuifunga nafsi yako, punguza hiyo hukumu na upe mwili wako nafasi ya kufanikiwa, ni kuamini kwamba unaweza, kuondoa mambo yasiyo ...

ZINGATIA HAYA KABLA YA KUANZA BIASHARA YA MTANDAO.

Image
Habari yako ndugu msomaji wa makala zangu za kila siku, ni siku nyingine tena tunakutana hapa nami Mkufunzi wako Frank A. Ndyanabo-FAN Nimekuwa nikikutana na watu mbali mbali, kwa sms, simu, na inbox ya hapa facebook na kwenye mitandao mingine kama kwenye blog yangu ya www.fancompany.blogspot.com, instagram, whatsapp, telegram na LinkedIn wakiniuliza juu ya biashara hii ya mtandao, ila nilikuwa nikiwaambia mambo mbali mbali juu ya biashara hii na mambo ya kufanya ili biashara zao ziweze kunawili na kuwaletea matunda walio yatarajia.  Leo napenda nikushilikishe kitu muhimu sana wewe ndugu yangu mfuatiliaji wa makala zangu hizi, ninaamini kati yenu wapo wanaofanya biashara hii na wengine wako mbioni kuingia na wengine wanatamani kuingia ila hawajuhi waanzie wapi. Kwanza hebu kwa ufupi tufahama biashara ya mtandao ni nini: Biashara ya mtandao au kwa lugha nyingine wanaita biashara ya karne ya 21, ni mfumo wa biashara ambao unamuwezesha mtu kufanya biashara huria kwa kununua bidhaa...