Posts

Showing posts with the label makala

MAISHA NDIVYO YALIVYO

Image
Lazima kuwe na Equity and Justice . 

THERE IS NO FUTURE IN THE PAST

Image
THERE IS NO FUTURE IN THE PAST. Ukitaka kufanikiwa usiangalie nyuma yako kunanini na ulishindwa mara ngapi. Siku zote kukaa Chini nakuanza kujuta kwa makosa uliofanya uko nyuma nikupoteza muda, huo muda Utumie kwa kupanga ya kesho. Bahati nzuri Mungu alitujalia kusahau, ivyo siku zote sahau ya nyuma na waza yale ya mbele yako. Maisha bora ya mbele hayawezi kuja kama akili yako imebeba kushindwa kwa nyuma. Binadamu yeyote anayeweza kupoteza muda wake wa leo kwa kulaumu mabaya ya jana, kesho atapoteza muda akilaumu mabaya ya leo. Tambua ya kuwa, "hakuna awezaye kurudi nyuma na kuanza upya, bali waweza kuanza leo na kutengeneza maisha yako ya kesho" Kadri unavyofikiria ya nyuma ndivyo unavyochelewa kufika mbele zaidi. Penda zaidi ndoto yako ya kesho kuliko historia yako ya jana,maana hatima yako siku zote iko mbele na sio nyuma. Siku zote utashindwa kwa kuendekeza mambo yaliopitwa na wakati maana utakuwa unatumia ujuzi uliopitwa na wakati. "Habari njema ya siku ni ...

TANGAZO LA AJIRA

Image
TANGAZO LA AJIRA. NYUMBANI BUSINESS PLAN ENTERPRISES Inakutangazia nafasi ya kazi katika idara ya afisa mauzo kwa watu wote waishio MWANZA. SIFA ZA MUOMBAJI. ••Awe ni muhitimu wa kidato cha nne Au sita. ••Awe na shahada,stashahada au cheti cha Masoko(marketing), Sayansi ya jamii(sociology), usimamizi wa biashara(business administration), fedha (finance), kibenki(banking) KAZI ZA AFISA MAUZO. 1.Kutafuta na kutengeneza masoko mapya ya bidhaa. 2.Kuandaa taarifa ya mauzo kila siku, kwa wiki na mwezi. 3.Kufuatilia na kukusanya mauzo ya kila siku. 4.Kutoa taarifa ya utendaji kazi kwa msimamizi(supervisor) wake kila siku. MSHAHARA MNONO UTATOLEWA TUMA MAOMBI: Tuma maombi yako kwenda kwa Afisa Utumishi wa Nyumbani Business Plan. Email: nyumbanibusinessplan@gmail.com Kwa Mawasiliano zaidi. • +255 753 183 583 • +255 684 459 947 MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 30/06/2016

ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO.

Image
ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO. SEHEMU YA 2. Karibu katika mwendelezo wa mada yetu iliyotangulia ikiwa na sehemu ya kwanza na leo tuko katika sehemu ya pili. Kila mtu anatamani maisha yake yabadilike kutoka alipo na kusonga mbele zaidi. Ila maisha hubadilika pale tu unapotaka yabadilike. Na ili yaweze kubadilika lazima ukubali kupigika kwa ajili ya kuyafanya yabadilike.  Huwezi kulala na kuamka ukakuta yamebadilika. Kwa leo hebu tujifunze njia zingine : 6. Achana na mahusiano yenye kukuumiza. Watu wengi naweza sema ni ving'ang'anizi kwa mambo yasiyo na tija.  Haimaanishi kuwa, kwakuwa umekuwa na mtu au umekuwa ukifanya jambo fulani kipindi cha nyuma basi ni lazima uwe nae au uendelee na mambo hayo maishani mwako. Kukosa jambo fulani ulilolizoea haimaanishi kuwa lazima ulipate.  Au kumkosa mwenzako aliye kuumiza hapo awali haimaanishi kuwa lazima uwe nae maishani mwako.  Kukikosa kitu cha awali ni nafasi nzuri kwako kupata muda wa kusonga mbele k...

UNAJIFUNZA NINI KUTOKA KWA BINTI GETRUDE CLEMENTI?

Image
UNAJIFUNZA NINI KUTOKA KWA BINTI GETRUDE CLEMENTI? Getrude Clement ni binti kutoka Jijini Mwanza, nchini Tanzania.  Na anasoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari Mnarani, ilioko nje kidogo ya mji takribani km 10 au zaidi kutoka mjini. Shule iyo ni ya serikali ni moja kati ya shule za kata zilizoanzishwa kipindi hicho. Getrude ana umri wa miaka 16. Alipata fursa ya kipekee kuongea kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa, akikaribishwa na Mhe. Ban Ki Moon, katibu mkuu wa umoja wa Mataifa kama muwakilishi wa watoto na vijana wote duniani kwa ajili ya kuzungumzia maswala ya mazingira na uchafuzi wake. Baba yake ni Kinyozi na mama yake ni mfanya biashara mdogo mdogo wa nyanya na vitunguu. Getruda Clement, aliweza kuushangaza ulimwengu jinsi alivyo simama mbele ya viongozi mbali mbali nakuweza kuhutubia bila wasi wasi na kwa kujiamini kupita kiasi.  Ujasiri alio nao binti huyu ndio umenifanya niandike maneno haya ili uweze kujifunza kitu fulani. Wewe kama mfuatiliaji mzuri wa...

ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO.

Image
ZIFAHAMU NJIA SAHIHI ZA KUBADILI MAISHA YAKO. SEHEMU YA 1: Kila mtu anatamani maisha yake yabadilike kutoka alipo na kusonga mbele zaidi.  Ila maisha hubadilika pale tu unapotaka yabadilike. Na ili yaweze kubadilika lazima ukubali kupigika kwa ajili ya kuyafanya yabadilike.  Huwezi kulala na kuamka ukakuta yamebadilika. Leo nimeamua kukuletea njia zitakazo fanya maisha yako yabadilike kikamilifu endapo utayazingatia.  Siku zote ndoto yangu mimi Frank A. Ndyanabo - FAN ni kuona kila ninacho kifanya kinaleta matunda chanya kwa watu hasa wewe unayesoma na kufuatilia makala zangu hapa kila siku.  Ila ndoto hii na furaha yangu haiwezi kukamilika kama hautawashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako ili na wao wapate ujumbe huu. Sasa hebu njoo tutembee pamoja tujifunze mambo haya. 1. Ondoa mambo mabaya maishani mwako. Ukiona kitu fulani hakikuongezei thamani au hakina manufaa maishani mwako huna budi kukiacha.  Huwezi kupata maisha mapya bila kukubali kuachana na ...

MATENDO NI TIBA YA WOGA.

Image
MATENDO NI TIBA YA WOGA. Hii ndio dawa pekee ya kutibu ugonjwa wa woga ndani yako.  Pindi tunapotaka kufanya jambo fulani utakuta tunakabiliwa na woga. Woga ni kitu kibaya sana katika maisha yetu ya kila siku. Jiulize ni mambo gani umeshindwa kuyafanya kwa sababu ya woga. Siku zote ukitaka kushinda jambo kwanza ondoa woga ndani yako.  Na ili kufanikisha jambo lako jiulize ni kitu gani ufanye ili kukabiliana na woga uliopo ndani yako. Jibu utakalolipata litumie kukabiliana na adui huyo woga.  Utakuwa umepata muarobaini wa mafanikio yako. Weka mfumo mpya sasa wa maisha yako, utakaokupa mwanga sahihi katika maisha yako.  Utakuwa umekutana na fursa nyingi katika maisha yako ila woga umekufunika na kuiteka akili yako.  Sasa ni wakati wa kukataa hali hiyo na kuamua kutenda. Nyanyuka tutembee pamoja sasa. By: Frank A. Ndyanabo - FAN

UMRI WAKO SIO KIKWAZO.

Image
Watu wengi tumekuwa tukipata kigugumizi juu ya maamuzi yetu katika kuzielekea ndoto zetu.  Wapo tunaofikiria umri wetu kutujengea vikwazo mbele yetu.  Umri wako kuwa mkubwa sio sababu ya kukuzuia kutimiza ndoto yako.  Nimekuwa nikikutana na watu mbali mbali na kuwashirikisha juu ya fursa za kuwaletea maendeleo lakini hutanguliza swala la umri mbele.  Utasikia mtu anakwambia, "mimi umri umekwenda nimeisha jichokea na karibia nitakufa"  Aliyekwambia utakufa kesho au baada ya mwaka mmoja ni nani?  Umri wa uzalishaji kwa mwanadamu hasa Tanzania ni miaka 60.  Sasa utakuta mtu ana miaka 40 anakwambia umri wake umeenda na hawezi kufanya jambo lolote kwa sababu ya umri.  Sasa kama una miaka 40, hujui kuwa bado una miaka 20 mbele?  Kwa maana hiyo umeisha tumia 50% ya maisha yako katika utafutaji hapa duniani. Toka ulivyo timiza miaka 20 nakuanza kujitengenezea maisha, ulikuwa na jukumu la miaka 40 mbele, hivyo bado unadaiwa asilimia 50 mbele yako....

JIFUNZE JAMBO HILI KILA SIKU.

Image
Mzee mmoja alianza hofia kuwa yawezekana mkewe kaanza matatizo ya kutosikia vizuri.Hivyo ikambidi amtafute daktari wa familia na kumsimulia mkasa mzima. Baada ya daktari kumsikiliza yule mme vizuri, akamwambia kuwa sasa atahitaji akirudi nyumbani amfanyie jaribio moja mkewe ili majibu yake yaweze kumpa dokta mwanga wa kumsaidia kulitambua tatatizo na yule mama apone. Daktari akamwambia, “ ukirudi nyumbani simama futi 40 kutoka kwa mkeo na kwa sauti ya mazungumzo ya kawaida ongea neno ili uone kama atasikia na kama hatasikia simama karibu futi 30 ukimsogela , kama hatishoshi ongeza zaidi futi 20 mpaka atakapo kusikia” Jioni yake mzee akiwa sebuleni na mama akiwa jikoni anaandaa chakula cha jioni, baba akiwa sebuleni akamwita mkewe na kuuliza, “Mpenzi tuna kula nini leo jioni?” lakini mke hakujibu. Mzee akazidi kusogea futi 30 karibu akamuuliza tena, “Mpenzi tuna kula nini leo jioni?” lakini pia mke hakujibu, mzee akasogea tena fu...

ZINGATIA HAYA KILA SIKU.

Image
ZINGATIA HAYA KILA SIKU. Yaweza kuwa unayafahamu ila hujui umuhimu wake, au unajua ila unayachukulia kawaida sana.  Lazima ufikie mahali ujiulize ni kwa kiasi gani unazitumia mbinu hizi kimaendeleo. Hizi ndio waswahili usema "nondo nzito"  ila mimi nasema ni "funguo tatu muhimu katika maisha yako"  funguo hizi ukipoteza moja wapo basi usitegemee muujiza, Maana mafanikio hayamfuati mtu kama muujiza bali mtu mwenye ndio uyafanya yamtokee kama muujiza kwake.  Na funguo hizi ndio za kutumia ili ufikie pale ulipopalenga. MTANGULIZE MUNGU KILA SIKU: Najua kila mtu ananjia yake ya kuabudu, uwe Mwislam au mkristu unamuabudu Mungu alie juu, basi tambua kuwa ata uwe mjanja namna gani Mungu ndio kilakitu.  Huwezi kufanikiwa bila kumuweka mbele.  Nakumbuka wakati nikiwa shuleni, na nikiwa kiongozi wa dini kwa wanafunzi kimkoa tulikuwa na usemi wetu kuwa "God.... first, education..... Second"  hii inamaana kuwa katika mambo yote utakayoyafanya lazima Mungu umtan...

HACHA KUIHUKUMU NAFSI YAKO

Image
HACHA KUIHUKUMU NAFSI YAKO. Kila mtu analo jambo la kufanya na tunayo malengo ya kutimiza, ila tatizo ni kuwa mioyo yetu imejaa hukumu zisizo za msingi ndio maana tunashindwa kutimiza malengo yetu.  Tunatanguliza kushindwa, aliekwambia kuwa huwezi kumiliki biashara yako nani, nani alikwambia kuwa huwezi kumiliki kampuni?  Nani alikwambia huwezi kuwa kiongozi bora, unafikiri mafanikio watu wanazaliwa nayo?  Yote yanatafutwa hapa hapa duniani.  Hacha kujihukumu bure kuwa huwezi jambo fulani,kwani wewe ni nani usiweze, wanaoweza wana nini cha ajabu? Biashara zetu zinashindwa kustawi kutokana na minyororo iliopo ndani yetu maana tumeifunga kisawa sawa.  Mtu wazo la kufanya biashara au jambo fulani unalo ila hutaki kufanya unategemea nani akufanyie sasa, au unataka jirani yako aje afanye badala yako?  Hachana  na mawazo hayo ya kuifunga nafsi yako, punguza hiyo hukumu na upe mwili wako nafasi ya kufanikiwa, ni kuamini kwamba unaweza, kuondoa mambo yasiyo ...

ZINGATIA HAYA KABLA YA KUANZA BIASHARA YA MTANDAO.

Image
Habari yako ndugu msomaji wa makala zangu za kila siku, ni siku nyingine tena tunakutana hapa nami Mkufunzi wako Frank A. Ndyanabo-FAN Nimekuwa nikikutana na watu mbali mbali, kwa sms, simu, na inbox ya hapa facebook na kwenye mitandao mingine kama kwenye blog yangu ya www.fancompany.blogspot.com, instagram, whatsapp, telegram na LinkedIn wakiniuliza juu ya biashara hii ya mtandao, ila nilikuwa nikiwaambia mambo mbali mbali juu ya biashara hii na mambo ya kufanya ili biashara zao ziweze kunawili na kuwaletea matunda walio yatarajia.  Leo napenda nikushilikishe kitu muhimu sana wewe ndugu yangu mfuatiliaji wa makala zangu hizi, ninaamini kati yenu wapo wanaofanya biashara hii na wengine wako mbioni kuingia na wengine wanatamani kuingia ila hawajuhi waanzie wapi. Kwanza hebu kwa ufupi tufahama biashara ya mtandao ni nini: Biashara ya mtandao au kwa lugha nyingine wanaita biashara ya karne ya 21, ni mfumo wa biashara ambao unamuwezesha mtu kufanya biashara huria kwa kununua bidhaa...

JIFUNZE KUTUMIA PESA

Image
JIFUNZE KUTUMIA PESA. Habari yako ndugu msomaji wa makala zangu za kila siku.  Natumai ni mzima wa afya tele.  Leo nakuletea mada ambayo nimeona ni tatizo kwa watu wengi, hivyo karibu uweze kujipatia somo hili makini na lenye Mwanga wa maisha yetu. Ulisha jiuliza kwa nini maskini wanazidi kuwa maskini zaidi na matajiri wanazidi kuwa matajiri?  Kuna msemo mmoja nimekuwa nikiusikia toka nikiwa mtoto mdogo, kuwa  ukizaliwa maskini basi utakufa maskini na tajiri atazidi kuwa tajiri.  Bado wakaenda mbele zaidi kuwa mwenye nacho atazidi kuongezeawa, hapa tunasema maji ufuata mkondo, haipo siku maji yakapanda mlima.  Kauli hizi zinaweza kuwa kweli au si kweli, Je wewe kutokana na mtazamo wako unaonaje? Kwangu mimi Frank, nasema sio kweli kabisa matajiri wanaendelea kuwa matajiri kwa maana wanajua mbinu sahihi za kutumia pesa hili kutengeneza pesa ndio maana pesa kwao hazikatiki.  Lakini kumbuka watu hao hawakuzaliwa wakiwa matajiri bali nao walikuwa maskin...

JINSI YA KUANZA BIASHARA BILA MTAJI. SEHEMU YA 2

Image
JINSI YA KUANZA BIASHARA BILA MTAJI. SEHEMU YA 2 : Habari yako ndugu msomaji wa makala zangu, natumaini ni mazima wa afya.  Nikukaribishe katika mwendelezo wa darasa hili ambalo leo tunaingia sehemu ya pili, ili kuweza kutazama mambo gani yanaweza kutusaidia ili kuweza kuanza biashara zetu bila mtaji.   Utakuwa nami Mkufunzi na Mshauri wako wa maswala ya biashara, Frank A Ndyanabo. Karibu twende pamoja: TUMIA ELIMU YAKO (USE YOUR KNOWLEDGE) Hili limekuwa ni tatizo kubwa kwa tulio wengi.  Tunapomaliza shule tunawaza kuajiriwa, ulisha jiuliza kiwango cha wahitimu na idadi ya ajira zilizopo? Takwimu zinaonyesha kuwa ajira ni chache ukilinganisha na idadi ya wahitimu wa vyuo nchini hasa apa Tanzania.  Nakumbuka mwaka juzi zilitangazwa nafasi za kazi uhamiaji, walioshiliki katika interview ya hawali walikuwa ni maelufu ya watu mpaka mamlaka husika wakakosa mahali pakuwaweka wakawapeleka uwanjani wa taifa. Sasa jiulize kama interview inafanywa na watu zaidi ya 25...

JINSI YA KUANZA BIASHARA BILA MTAJI. SEHEMU YA 3

Image
JINSI YA KUANZA BIASHARA BILA MTAJI. SEHEMU YA 3. Habari yako ndugu msomaji wa makala hii.  Tuko katika mwendelezo wa mada yetu ya, kuanza biashara bila mtaji.  Na leo tunaendelea na sehemu ya tatu ya mada hii, leo tutaangalia mambo mawili ambayo unaweza kuyatumia na yakakusaidia katika kuanza biashara.  Karibu tujumuike sote. TUMIA UWEZO BINAFSI. Katika hali ya kawaida kila mwanadamu kajaliwa uwezo fulani wa ziada ambao mbali na elimu au kipaji cha kuzaliwa nacho ila anaweza kuwa kajaliwa uwezo fulani binafsi ambao unaweza kuupata kwa kufanyia mazoezi kila mala na ukaweza kubobea katika jambo hilo. Sasa basi kama wewe ni mbobevu katika jambo fulani basi waweza kutumia nafasi hiyo nakuweza kujitengenezea mfereji wa pesa.  Mfano: yawezekana wewe ni mbunifu wa mitindo mbalimbali ya mavazi, basi fungua office au kampuni kisha anza kuonyesha umahili wako katika kubuni mavazi na mitindo mbalimbali. Au yawezekana wewe ni mchoraji mzuri, kiasi kwamba ukiamua kuchora b...

JINSI YA KUANZA BIASHARA BILA MTAJI.

Image
JINSI YA KUANZA BIASHARA BILA MTAJI. SEHEMU YA 1: Habari yako ndugu msomaji wa makala zangu.  Ni siku nyingine tunakutana hapa kwa ajili ya kuelimishana na kupeana maarifa kwa ajili ya kutoka katika janga hili la umaskini na kujikomboa kifikra. Ashukuriwe Mungu alie juu, kwa kuendelea kuniweka hai mimi Frank A. Ndyanabo, natumai nawe ni mzima wa afya. MUNGU wetu ni mwingi wa rehema na ndio maana kila mtu kamjalia karama mbali mbali.  Na mimi Frank, kanijalia kipaji cha kukuelimisha wewe, na pia kwa kujua kuwa wewe ni muhimu sana kakujalia akili ambazo ndio mtaji mkubwa katika maisha yako.   Kwa mantiki hiyo akili ndio chanzo cha mambo yote, tunapoenda katika mada yetu tutaona jinsi gani Mungu huyu alivyo na makusudi yake katika hili. Kila mtu ameumbiwa utajiri na akili ila tunatofautiana katika matumizi tu.  Katika kuanza biashara unatakiwa kuumiza sana kichwa kwa kuishughulisha akili yako ili uweze kushinda,  haipo siku hata moja ambayo utamsikia mtu ...

KUWA KIOO KWA WENGINE.

Image
KUWA KIO KWA WENGINE.  Kioo siku zote utoataswila sahihi ya kile kilichoko mbele yake. Kama mwanamke akisimama mbele ya Kioo haiwezi kuonekana taswira ya mwanaume kwenye kio. Hii inakupa picha kuwa siku zote utabaki kuwa wewe kama wewe tu. Vyovyote utakavyo jiweka ndivyo utakavyo onekana.  Swali la kujiuliza, Je unataka uonekaneje katika Kioo ? Ukitaka maisha yako kuwa mazuri basi kuwa Kioo kwa wengine.  Chochote utakacho panda kwao ndio utakacho vuna.  Kama wewe unaishi na watu vizuri basi na watu watakupenda na kinyume chake inawezekana.  Ukitaka kupokea zaidi basi na wewe toa zaidi.  Kuna msemo mmoja zamani kutokana na akili za katoto sikuuelewa vizuri nilikuwa nikiutafsiri kitoto, msemo huo unasema hivi "Ukitaka kula shariti nawe uliwe kidogo"  hii kauli inamaana kubwa sana.  Ata maandiko yanasema, huwezi kukusanya husipo Tapanya, yaani kwa lugha nyingine huwezi vuna usipo panda.  Ivyo basi kama unaitaji mambo mazuri nawe wekeza katika...

AMKA SASA NA JIPANGE, DUNIA INAKIMBIA WAKATI WEWE UNATEMBEA.

Image
Great advice from the Richest person in China Mr. Jack Ma. Jack Ma says, "Please tell your children that the world is changing every day and no one is going to wait for you in the past. When lighter was invented, matches slowly disappeared. When calculator was created, abacus was to fade away. When digital camera was designed, the market of negative film no longer existed. When direct market selling/internet-based selling arises, traditional marketing declines. When smartphone with 4G (wireless internet access) was introduced to the world, you no longer need to turn on your computer at home. When WeChat and WhatsApp (mobile text/voice/video messaging) are developed, traditional text messaging is no longer as popular as before. Let's not to blame "Who took over Whose business." It's only because people are more adjustable and adaptable to new ideas and changes in the world. Someone asks Jack Ma, "What is your secret for success?" He says, "Really...

JIFUNZE JINSI YA KUPATA WAZO LA BIASHARA. SEHEMU YA 2.

Image
JIFUNZE JINSI YA KUPATA WAZO LA BIASHARA.  SEHEMU YA 2 Baada ya kuwa tumeona zile njia tatu za awali, basi apa tutaona njia zingine ambazo zitakusaidia kupata wazo la biashara kama una ndoto za kuanzisha biashara. Kwa dondoo tu kwa zile tulizokwisha jifunza, tuliona jinsi ya kukitumia kipaji chako kama wazo la biashara, kwa kutumia shida zilizopo katika jamii yako na kuwa wazo la biashara na mwisho tukaona jinsi ya kujifunza kutoka kwa watu mbalimbali waliokwisha kutangulia.  Basi tutazame mbinu zingine unazoweza kutumia na kupata wazo la biashara. KUPITIA MAZUNGUMZO YA MARAFIKI ZAKO. Kila mtu anamarafiki wa aina mbalimbali ivyo kupitia wao unaweza pata wazo la biashara.  Chamsingi angalia ni mambo gani wanapendelea kuzungumza na wanapendelea nini.  Ukiona wanapendelea mambo fulani na ili wayapate uwalazimu kutumia gharama na muda MWINGI kuyapata.  Basi wewe kuwa suluhisho la tatizo lao, kisha utaona utakavyo pata pesa mpaka ushangae.  Mfano kwa akina...

JIFUNZE JINSI YA KUPATA WAZO LA BIASHARA.

Image
JIFUNZE JINSI YA KUPATA WAZO LA BIASHARA. Habari yako ndugu msomaji wangu, natumai umejaariwa afya tele na Mwenyezi Mungu.  Vivyo hivyo na mimi anazidi kunijalia pumzi ili niendelee kutimiza lengo lake la kuniletea duniani.  Najua moja ya lengo lake ni kunifanya nikuelimishe juu ya mambo mbali mbali ya maisha hasa yale yanayolenga kukuza uchumi wako wa kila siku.  Leo nakuletea mada nzito iliosheheni utamu na ufumbuzi wa matatizo mengi hasa kwetu sisi wenye ndoto ya kuwa wajasiriamali na wawekezaji wakubwa hasa katika ulimwengu huu wenye utandawazi wa technologia kubwa.  Katika ulimwengu huu, kiujasiriama umegawanyika katika makundi makuu matatu. ▶ Watu wenye pesa lakini hawana muda na hawana wazo la biashara. ▶Watu wenye muda lakini hawana pesa wala wazo La biashara. ▶Watu wenye wazo la biashara lakini hawana muda wala pesa. Basi leo nitajikita hasa katika swala la kujua jinsi gani mtu unaweza kupata wazo la biashara. Kuna njia nyingi sana z...